News

𝐊𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐉𝐈: 𝐌𝐀𝐀𝐅𝐈𝐒𝐀 𝐍𝐀 𝐀𝐒𝐊𝐀𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐇𝐈𝐅𝐀𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐁𝐔𝐑𝐈𝐆𝐈 - 𝐂𝐇𝐀𝐓𝐎 𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐄𝐍𝐈 𝐊𝐔𝐈𝐌𝐀𝐑𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐒𝐇𝐔𝐆𝐇𝐔𝐋𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐇𝐈𝐅𝐀𝐃𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐋𝐈𝐈

​Kamishna wa Uhifadhi Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Musa Nassoro Kuji, amehimiza maafisa na askari wa Hifadhi ya Taifa Burigi - Chato kuwajibika kikamilifu katika kuboresha na kuimarisha shughuli za uhifadhi na utalii. Read More

Posted On: Mar 16, 2025

​KAMISHNA KUJI AHIMIZA UADILIFU NA USHIRIKIANO KATIKA KUIMARISHA UHIFADHI KISIWA CHA RUBONDO

Kamishna wa Uhifadhi - TANAPA Musa Kuji amewataka Maafisa na Askari wa Uhifadhi katika Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Rubondo kufanya kazi kwa uadilifu, weledi, bidii, nidhamu pamoja na ushirikiano ili kutimiza adhima na malengo ya kuimarisha shughuli za uhifadhi katika Hifadhi ya Taifa Kisiwa cha Rubondo. Kamishna Kuji aliyasema hayo jana Machi 15, 2025 alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua shughuli mbalimba na kufanya kikao na Maafisa na Askari hao katika ofisi za Makao Makuu ya hifadhi hiyo yaliyopo eneo la Kageye ndani ya Hifadhi hiyo iliyopo katika Mkoa wa Geita. Read More

Posted On: Mar 16, 2025

UJENZI DARAJA LA MTO KOGATENDE: SULUHU YA KUDUMU KWA UTALII NA UHIFADHI ENDELEVU SERENGETI

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Jenerali (Mst.) George Marwa Waitara ameiagiza Menejimenti ya TANAPA kuhakikisha kuwa ujenzi wa daraja la Mto Kogatende unakamilika kwa wakati na kwa ubora ili kuruhusu shughuli za uhifadhi na utalii kuendelea. Read More

Posted On: Mar 14, 2025

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YAPONGEZA JUHUDI ZA WIZARA KUPITIA TANAPA KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI HIFADHINI.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa hatua kubwa walizofanya katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ndani ya Hifadhi ya Taifa Tarangire ambayo itawezesha watalii wengi kufika kwa urahisi ndani ya hifadhi hiyo. Kamati hiyo imetoa pongezi hizo leo Machi 12, 2025, katika ziara yake ya ukaguzi wa mradi wa Lango la kuingilia watalii la Mamire katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire pamoja na ukarabati wa barabara mbalimbali zilizoko ndani ya hifadhi. Read More

Posted On: Mar 13, 2025

𝐓𝐀𝐍𝐀𝐏𝐀 𝐂𝐞𝐥𝐞𝐛𝐫𝐚𝐭𝐞𝐬 𝐅𝐢𝐯𝐞 𝐂𝐨𝐧𝐬𝐞𝐜𝐮𝐭𝐢𝐯𝐞 𝐖𝐢𝐧𝐬 𝐨𝐟 𝐐𝐮𝐚𝐥𝐢𝐭𝐲 𝐂𝐡𝐨𝐢𝐜𝐞 𝐏𝐫𝐢𝐳𝐞 𝐟𝐨𝐫 𝐄𝐱𝐜𝐞𝐥𝐥𝐞𝐧𝐜𝐞 𝐢𝐧 𝐒𝐞𝐫𝐯𝐢𝐜𝐞 𝐃𝐞𝐥𝐢𝐯𝐞𝐫𝐲

Tanzania National Parks (TANAPA) has been honored with the prestigious Quality Choice Prize 2024 in recognition of its exceptional commitment to delivering world-class services within and beyond the organization. The award ceremony, organized by the European Society for Quality Research (ESQR), took place on December 9, 2024, at Parkhotel Schönbrunn in Vienna, Austria. The award was received by the Deputy Minister of Natural Resources and Tourism for Tanzania, Hon. Dustan Kitandula, who was accompanied by Ambassador of United Repblic of Tanzania in Vienna Austria, Hon. Naimi Aziz, TANAPA’s Conservation Commissioner Musa Juma, Western Zonal Senior Conservation Commissioner Izumbe Msindai, Conservation Commissioner’s Personal Assistant Andrew Mbai, and Conservation Officer from the Business Development Section, Daniel Mweta. Read More

Posted On: Dec 10, 2024

ZAIDI YA WATANZANIA 230 KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU KATIKA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO

Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeongoza Watanzania na wapandaji wengine zaidi ya 230 kutoka mataifa ya China, Marekani na Ufaransa leo Desemba 05, 2024 kupanda Mlima Kilimanjaro kupitia Lango la Marangu lililopo mkoani Kilimanjaro. Watu hao wamepanda mlima huo kwa lengo la kwenda kupandisha Bendera ya Tanzania ikiwa ni ishara ya kumbukumbu ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika. Read More

Posted On: Dec 06, 2024